Kusema HAPANA kuliokoa maisha yangu

Usiogope kusema hivyo!

Maria kutoka darasa la juu alitualika mimi na rafiki yangu Carolina kwenye sherehe na wanafunzi wengine wakubwa. Tulikuwa na raha tele huku tukicheza, kuzungumza na kutulia. Tulipoteza usawaziko na kutambua ilikuwa karibu usiku wa manane! Tungepaswa kuondoka wakati huo ikiwa tungetaka kupata basi la mwisho kurudi nyumbani.

Maria na marafiki zake wakubwa walinisikia nikimwambia Carolina kwamba ilitubidi tuondoke ili tupate basi. Walituambia kwamba hatungeweza kuondoka, kwamba sherehe ilikuwa ndio inaanza. Nilimwambia hatungekosa basi la mwisho, ama sivyo hatungekuwa na njia yoyote kwenda nyumbani. Walianza kututilia shinikizo kwa kusema kuwa sisi tulikuwa hatufurahishi.

Carolina alinisimamia na kusema kuwa kurudi nyumbani baadaye kungekuwa hakufurahishi, na ingechukua muda mrefu!

Ilikuwa wazi Maria alikuwa amelewa kiasi na hakukata tamaa. Mimi na Carolina tulikwua tumelemewa. Tulikuwa na wakati mzuri, na hatukutaka kuonekana kama wachanga na wasiofurahisha mbele za wakubwa. Lakini tulijuwa kwamba kurudi nyumbani usiku ilikuwa hatari sana na basi ndio njia pekee salama kwenda nyumbani.

Hata ingawa tulikuwa na wasiwasi, mimi na Carolina tulikuwa na msimamo. Tulisema hapana kwa kukaa tena na tukamwambia Maria na marafiki zake kwamba sisi tunaondoka. Tulikuwa na wasiwasi jinsi ambavyo Maria angeweza kufika nyumbani – hivyo tulianza kumwambia kwamba anapaswa kutoka pamoja na sisi. Wavulana wote wakubwa walianza kucheka. Mimi na Carolina tulijua kwamba tulihitaji kumchunga Maria na hatukujali tulivyoonekana kwa wale wavulana wakubwa. Kufika nyumbani salama na kumchunga rafiki yetu ilikuwa muhumu zaidi kuliko masaa machache zaidi kweye sherehe!

Baada ya mvutano, Maria alikubali kwamba angejiunga nasi kwenye basi la kwenda nyumbani.

Ingawa nilikuwa na wasiwasi kuwasimamia wakubwa wale na kumwambia Maria cha kufanya, nilijua ilinibidi. Tulipata basi kwa chini ya dakika. Siku iliyofuata tulisikia habari kwamba kulikuwa na wizi kwenye barabara ambayo tungetembelea usiku huo. Kusema hapana kuliokoa maisha yetu na Maria pia alishukuru tulimpeleka nyumbani.

Share your feedback