Vyakula visivyo na madini yanayofa havipo!

...Na wakati wa kula lishe bora umefika! Ni wakati wa kujitunza inavyofaa.

Vijana wana mengi ya kufanya kila siku, kutoka shuleni hadi kwenye vikundi vya kusoma hadi kwenye spoti na shughuli nyingine zisizokuwa za darasani, kumlea mtoto na kusaidia kwa kazi za nyumbani. Haishangazi kuwa mwili wako unahitaji nguvu nyingi sana, lakini unahitaji kuupa nishati!

Vijana wanahitaji madini mazuri na ingawa vibanzi na vinywaji baridi vinaweza kuwa na ladha nzuri, si vizuri kwa mwili wako unaokua. Ni vibaya sana kwa afya yako, hivyo ukiacha kunywa vinywaji vyenye sukari mapema na kuanza kufanya maamuzi mazuri ya chakula, utahisi vizuri. Ni rahisi kuliko unavyofikiri, msichana!

Kwa nini ule vizuri?
Ingawa inaonekana ni kama unaweza kula chochote, kwa mfano vyakula vya kupikwa haraka vikiandamana na barafu kwa chajio na usiongeze uzani, maamuzi mabaya ya kula yana athari kwenye maisha yako. Mwili wako unahitaji madini mengi sana ili kuendelea kukuza mwili na akili zako — na uendelee kuwa na nguvu. Kula matunda na mboga zaidi kutasaidia kukukinga dhidi ya ugonjwa na majeraha na kukuongeza nguvu kwa ajili ya masomo yako, kazi za nyumbani, na mambo yako unayopenda kuyafanya.

Mama anajua kilicho chema!
Hii inahusisha mambo ya jikoni pia. Mama amekuwa akikupikia milo mizuri yenye afya maishani mwako mote. Kwa hivyo ni nani bora wa kukusaidia kuanza maisha yako mapya ya kula vizuri? Msaidie anapoandaa milo jikoni ili kupata vidokezo vya vyakula na kupika, kama vile ni viungo vipi hutumika pamoja ili kuandaa mlo wenye lishe, jinsi ya kuongeza ladha kwenye nyama na mboga, na jinsi ya kupika kila kitu vizuri zaidi.

Maji ni rafiki yako wa dhati.
Si kinywaji kinachofurahisha wala kusisimua sana kwenye menyu, lakini maji ni kitu bora zaidi unachoweza kunywa. Ni muhimu sana kwenye afya yetu na mili yetu ina asilimia 60 ya maji. Tunahitaji kunywa maji kila mara kwa sababu tunapoteza viwango vikubwa vya maji wakati wa kutoka jasho, kuenda haja ndogo, na hata kupumua.

Ili kufanya maji yako kuwa ya kipekee bila kuongeza sukari wala kalori za ziada, jaribu kuongeza tunda au mboga, kama malimau au stroberi, kwa ladha nzuri. Au chukua soda na maji ikiwa unataka ile hali ya viputo vya gesi.

Haihusu tu Kula Chakula Chenye Lishe
Watu wanaposema mambo kama vile “Ninahitaji kupata lishe!” huwa hawajiulizi kwa nini, wala kufikiria kuhusu maana ya lishe. Mazungumzo mengi yanayotulenga sisi wasichana kuhusu lishe kwa kweli hayatuhusu sisi na afya na furaha yetu, yanahusu watu wengine wanaojaribu kutuambia jinsi tunavyopaswa kuonekana ili wapate pesa kutoka kwetu.

Kuwa na afya njema ni uamuzi unaojifanyia, kwa sababu unataka kuhisi vizuri na mwenye afya. Huli mboga na matunda zaidi kwa sababu mtu mwingine anataka ufanye hivyo. Unajifanyia! Ni kama kusema: “Hujambo mwili! Wewe ni mrembo sana na ninataka uwe na furaha. Kula tufaa.”

Hivyo... acha mambo mengi. Una mwili mmoja pekee! Upende na uufanye uwe na afya nzuri!

Share your feedback