Kuunda Pesa Zangu Binafsi

Jitahada yangu ya kujitegemea na kupata jaketi lenye thamani

Kuna msemo wa zamani: ‘pesa ni chanzo cha maovu yote’.

Ambapo ninasema: ‘LOL, unajua kiasi cha pesa cha jaketi lisilo la muda’.

Sawa, huenda hilo lisieleweke. Acha nifafanue.

Ninajua jinsi mama na baba yangu hujitahidi kila siku. Mama yangu huwa sokoni kila asubuhi. Baba yangu hufanya kazi ya usimamizi wa afisi na huhitajika kuondoka KABLA ya jua kuchomoza. Mimi si mjinga. Ninaheshimu jinsi wanavyojitahidi kunipa mimi na dada zangu wawili maisha mazuri.

Kwa hivyo ninapowaomba wazazi wangu pesa kununua kitu, sihisi kukosea tu. Huhisi vibaya sana. Kwa nini watie bidii kwa ajili yangu ili kuwa na kitu ambacho si lazima niwe nacho? Hii inaanzisha simulizi yangu ya kujitegemea kifedha kwa kuuza keki — yote kwa ajili ya kupata jaketi bora zaidi.

Sawa, si simulizi haswa. Au unajua, kusisimua. Lakini shangazi yangu huoka keki nzuri sana, ambazo huuza kwenye kibanda cha mama yangu sokoni. Hivyo, nilimwuliza ikiwa ningeenda na nyingine shuleni kuwauzia watoto wengine. Baada ya kunihoji kwa ukali na kwamba ikiwa ningeziuza kwa ugumu ningekuwa nikipoteza chakula na pesa, aliniruhusu kuchukua kumi.

Niliziuza asubuhi hiyo shuleni. Kisha nikafanya hivyo siku iliyofuatia. Na nyingine. Kisha wiki iliyofuata nikamwuliza shangazi yangu ikiwa angenipa ishirini. Kisha nikaziuza.

Kitu cha kwanza unachofahamu kwenye kazi yako ya kwanza? SALALE! UNA PESA ZAKO BINAFSI SASA. Kitu cha pili? Hupati hela nyingi, na unahitaji kutia bidii zaidi. Bila shaka hutatajirika kwa kuuzia marafiki zako keki shuleni.

Bado, hatimaye siku ilifika. Nilienda kwa mama yangu kwa kujivunia na kumwambia kuwa nilitaka kununua jaketi... lakini ni sawa, ningelilipia kwa pesa zangu binafsi! Nilijivunia sana. Nilikuwa nimemthibitishia mama yangu kuwa ningeweza kujitahidi na kujitegemea, kama tu yeye na baba walivyofanya.

Mambo ambayo sikutambua: hawakuwa na ukubwa wangu, hivyo nilinunua lile ambalo lilinibana kidogo na nikawa na umbo la kutisha sana nilipokuwa nyumbani. Na nililazimika kufanya kazi kwa wiki tatu ili kupata pesa. Kwa hivyo labda hayo hayakuwa matumizi mazuri ya pesa yangu.

Lakini, unajua jambo? Nilithibitisha kuwa ningeweza kufanya. Niliweka akiba pesa zangu. Nilichukua jukumu la kujishughulikia na kuwaondolea wazazi wangu mzigo. Na ninadhani kuwa siku moja, popote niendapo maishani, nitafikiria jaketi hilo na kukumbuka kuwa chochote unachokitaka maishani — haijalishi ni cha upuzi vipi! — ni kitu utakachohitaji kukitilia bidii.

Share your feedback