Usaidizi! Facebook yangu ilivamiwa!

Akaunti yangu ya Facebook inatuma ujumbe wa ajabu na sijui ni kwa nini. Inatuma vitu ambavyo havitoki kwangu. Marafiki zangu husema kuwa akaunti yangu ilivamiwa. Ni vipi ninavyoweza kulikomesha?

Mwaminifu, Aliyevamiwa na Mkosa Furaha

Mpendwa Aliyevamiwa na Mkosa Furaha,

Lo, mpendwa, ni kama akaunti yako ilivamiwa. Kwa maneno mengine, mtu ameingia katika akaunti yako na anachapisha ujumbe kwa niaba yako, akijifanya kuwa wewe. Wakati mwingine hili hutendeka ukisahau kuondoka katika akaunti yako kwenye Duka la Mtandao. Pia linaweza kutendeka ukiruhusu rafiki yako kuomba simu yako ya mkononi. Wakati mwingine ni wavamizi watalaam wanaoweza kuingia katika akaunti nyingi kwa kutumia mbinu za hali ya juu sana.

Wavamizi (wawe marafiki au watu usiowajua) huchapisha kutoka kwenye ukurasa au akaunti yako bila udhibiti wako. Wakati mwingine marafiki hufanya jambo hili kama utani, lakini ni muhimu kujaribu kupata udhibiti wa akaunti yako haraka uwezavyo!

Kwenye tovuti nyingi za mitandao ya jamii kama Facebook na Twitter unaweza kuripoti akaunti yako ikiwa imevamiwa. Ikiwa ilifanywa na marafiki wanaofanya mzaha, badilisha tu nenosiri lako na hilo pia linaweza kutatua tatizo.

Kila mara kumbuka kuondoka kwenye akaunti na uweke nenosiri lako salama, uwe unaingia katika akaunti kwenye duka la mtandao au simu ya mkononi ya rafiki. Huenda ikaonekana kutokuwa muhimu, lakini inaweza kukulinda dhidi ya mtu anayechapisha vitu kwa niaba yako vinavyoweza kuaibisha au kukuharibia sifa.

Kila heri unapotatua tatizo la uvamizi! Mpendwa, Bi. Tech

Share your feedback