Homoni! Hizo ni nini?

Jinsi ya kuwa na furaha na homoni!

Je, unapatwa na siku ambazo huwezi kabisa kukabiliana na hisia zako za mabadiliko? Je, umeona nywele mpya za mwili zikitokeza kwenye maeneo mapya? Au kuamka na ukasikia kama umekua inchi kadhaa katika usingizi wako? Au labda mvulana yule darasani amepunguza kuwa mchokozi na kawa mzuri zaidi – basi, umekisia vema, hizi ni homoni zako kazini!

Homoni ni wajumbe maalum wa kemikali katika mwili wako ambao huanza kuwia na kubadili wakati wa kubalehe.

Kwa wasichana wakati wa kubalehe, ovari zako huanza kutoa homoni zinazoitwa estrogen, progesterone na testosterone. Wakati mwili wako unaanza kutoa homoni hizi, matiti yako yataanza kukua, mwili wako utaanza kupata umbo na hedhi yako itaanza.

Kwa wavulana, viwango vya testosterone huongezeka – ndiyo sababu unaweza kusikia sauti yao ikiongezeka, kukua kwa nywele za uso na miili yao itakuwa mikubwa na mipana.

Inaweza kuwa ya kuchanganya kwa wasichana na wavulana kuelewa mabadiliko mengi ya kimwili na ya kihisia kwenye mwili wao wakati homoni zinafika. Nilipoanza kubalehe, niliongeza uzito, matiti yangu yalikua haraka sana kuliko ya marafiki zangu, na nilianza kujiuliza – “Je, hii ni kawaida?!”

Sikujua nizungumze na nani kuhusu hili. Nilikuwa na aibu sana kuuliza wazazi wangu, na dada yangu alikuwa mdogo kuliko mimi. Kwa bahati, muuguzi wa shule yetu alikuwa mzuri sana, na angeweza kunisaidia na maswali yoyote niliyokuwa nayo. Kama “Kwa nini ninasizi huzuni na kukasirika kabla ya hedhi yangu?” au “Kwa nini nina nia ya sukari sana wakati wa hedhi yangu?” Muuguzi alinifundisha kwamba kila mwili ni tofauti na hukaribia kubalehe katika hatua tofauti – lakini mabadiliko haya yote ni ya kawaida. Alisaidia kunifunza ukweli kuhusu homoni, badala ya kusikiza dhana nilizozisikia.

Jambo kubwa nililojifunza ni kwamba, kama hedhi yetu, homoni zetu hupitia mzunguko – hivyo ni muhimu kujifunza kukubali hisia zetu zinazobadilika na mahitaji katika mwezi wote.

Share your feedback