Saidia! Nina nywele

Nywele za mwili ni za kawaida na hutokea kwetu sote!

Enyi Spingster,

Nimeanza kugundua nywele katika sehemu ambazo sikuwa na nywele mbeleni. Nini kinatendeka? Nifanye nini kuhusu hilo?

Tafadhali saidia!

Amina


Ewe Mpenzi

Ahsante kwa swali lako. Kwanza, ni kawaida kabisa kwa nywele kuanza kumea katika sehemu za kila aina, kama kwenye makwapa yetu au kwenye uke wetu, tunapoanza kubalehe. Najua inaweza kuwa kitu kikubwa sana na hata yenye aibu, lakini ni jambo linalotokea kwa kila mtu. Inachanganya kuona miili yetu ikibadilika mbele ya macho yetu na wasichana wengi wana maswali mengi kuhusu mabadiliko haya.

Tunaita nywele inayokua kwenye uke wetu mavuzi na ni sehemu ya asili ya maisha. Inatokea kwa wavulana na wasichana tunapokuwa wakubwa na ni kawaida kama nywele zinazokua kutoka kichwani chako. Wasichana wengi wataanza kukua nywele kabla ya kuanza hedhi zao. Inaweza kuanza nyembamba na nyepesi lakini kwa kawaida huwa nyeusi zaidi na nene baada ya wakati. Watu wengine wanapendelea kuondoa nywele zao zote, na wengine hupenda kuzipunguza. Ni uchaguzi wa kibinafsi na hakuna njia sahihi au isiyo sahihi. Hakuna mtu anayepaswa kukuhimiza kutoa nywele zako, kwa sababu ni mwili wako, na hiyo inamaanisha ni uchaguzi wako.

Mavuzi ni afya. Inasaidia kuzuia bakteria hatari kuingia katika uke na kulinda midomo ya uke dhidi ya msuguano na usumbufu wa chupi yako.

Nywele za mwili ni sehemu ya asili ya maisha na sio kitu cha kuwa na aibu nacho. Ni moja ya mabadiliko mengi tunayopitia wakati wa ubalehe. Wakati wowote unahisi kuchanganyikiwa au kujisikia mwenyewe, daima wasiliana na rafiki au mtu wa familia anayeaminika na kumbuka hauko pekee yako.

Upendo mwingi

Dada yako mkubwa katika Springster

Share your feedback